Aabiria aliyefahamika kwa jina moja la Amina mkazi wa wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya alikufa papo hapo katika ajali iliyotokea juzi usiku katika Kituo cha Mabasi yaendayo Mikoani kutokea Mbeya baada  ya basi la New Force kuparamia ukuta wa mgahawa uliopo mkabala na Ofisi za Mabasi ya Kampuni hilo.

Tukio hilo limetokea majira ya saa 5:00 usiku wa Ijumaa ya Januari 20 mwaka huu  katika Kituo hicho cha Mabasi yakitokea mikoa mingine. 

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kondakta wa basi hilo aliyejulikana kwa jina la Januari Kapinga aliingia ndani ya basi hilo lenye namba za usajili T 853 AVQ aina ya Yutong lililokuwa likitokea Dar es Salaam baada ya abiria wote kushuka ndipo alipolikurupua kwa nguvu na kumshinda hatimaye kuparamia ukuta.

Abiria aliyefariki alikuwa safarini kuelekea masomoni mkoani Tabora na wakati gari likiparamia ukuta wa mgahawa huo alikuwa akipata chakula cha jioni. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi, mtu mmoja alifariki na watu watano kujeruhiwa.

Aidha kondakta wa basi hilo alitoroka na kwenda kusikojulikana na juhudi za Jeshi la Polisi kumtafuta zinaendelea. Dereva wa basi hilo anashikiliwa na Polisi kwa mahojiano zaidi.

Noah Mwakatumbula, Mwenyekiti wa Kituo cha Mabasi mkoani Mbeya yaendayo mikoani amewataka madereva waliopewa dhamana ya kuendesha vyombo hivyo na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waache mara moja tabia ya kuacha funguo za vyombo vyao vya usafi.

--
taarifa via blogu ya Mbeya Yetu
 


Comments

Gwamaka Isaac. M
23/01/2012 00:46

Ni jambo muhimu kwa madereva kuzingatia kanuni, dereva huwezi kumpa gari tingo aendeshe na unajua hana leseni au sio mzoefu. Madereva kuweni makini

Reply



Leave a Reply