Wafungwa wapatao 1300 nchini Kyrgyzstan wameshona midomo yao, huku wengine 700 wakiendelea na mgomo wa chakula ikiwa ni hatua ya kupinga hali mbaya na dhuluma wanazofanyiwa wakiwa gerezani.

Maofisa wa Kyrgyz wanasema kuwa wafungwa hao waliamua kushona midomo yao baada ya wakuu wa magereza kuwalazimisha kula ili  kuvunja mgomo wa kutokula waliouanza tangu Januari 17, 2012.

Kitendo cha kuwalazimisha kula kilisababisha ghasia baina ya wafungwa na askari ambapo inaripotiwa mfungwa mmoja alifariki dunia na wengine kujeruhiwa kiasi cha kupelekwa hospitali kwa matibabu.

Kyrgyzstan ilijipatia uhuru wake mwaka 1991 kutoka kwa Muungano wa nchi za Kisovieti uliovunjika. 

Inaripotiwa pia kuwa hali katika magereza ya nchi hiyo ya Bara la Asia ya Kati ni mbaya.
 


Comments




Leave a Reply