Serikali ya Tanzania imeufahamisha umma kuwa aliyekuwa kiongozi wa Libya ambaye sasa ni marehemu Muammar Qaddafi, binafsi hakuwahi kuwekeza kibiashara nchini Tanzania.

Akijibu swali la Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi, aliyetaka kujua Tanzania inanufaika vipi na uwekezaji wa kanali Muammar Gaddafi kibiashara, na kwa kuwa Tanzania haitambui serikali ya mpito ya Libya ni nani anayesimamia uwekezaji wa kibiashara wa marehemu kanali Muammar Gaddafi;  Waziri  wa nchi ofisi ya Waziri  Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Mary Nagu amesema kumbukumbu za kituo za uwekezaji zinaonyesha mradi mmoja tu ulioandikishwa kutoka  nchini Libya na kampuni ya NORTH AFRICA INVESTMENT TRADING COMMPANY  na si wa marehemu Qaddafi.

Akasema kampuni hiyo imeandika andiko la kibiashara la kuwekeza jumla ya dola za kimarekani milioni 5.8 na kutengeneza nafasi za ajira 160 pale ilipoinunua hoteli ya Bahari Beach iliyopo jijini Dar es Salaam.

source
 


Comments




Leave a Reply