Asasi ya kiraia Tweweza imezindua kampeni ya "Ni Sisi!" inayolenga kuwaamsha wananchi wa Tanzania kuhusu nafasi yao katika gurudumu la maendeleo. Kampeni hii inatumia majukwaa mbalimbali ya vyombo vya habari kutoa hamasa kuwa dhana ya mabadiliko kwenye jamii yanachangiwa kwa kiasi kikubwa na mwananchi mmoja mmoja, kinyume na kusubiri na kutegemea  serikali, wanasiasa, misaada, n.k.

Twaweza wanaamini kusimamia changamoto zinazotukabili na kushiriki kwa vitendo kwa wananchi ni vitu ambavo vinaweza kusukuma maendeleo endelevu.

Tazama video zifuatazo kuhusu sekta na maada mbalimbali kisha toa maoni yako. Itakuwa vizuri pia ukisambaza kwa Watanzania wengine.

1. Daladala/Matatu
2. Viwanja vya Michezo
3.  Huduma za Afya
4. Daraja
5. Uchafuzi wa Mazingira

6. Uteketezaji wa Misitu
 


Comments

mpekenyuzi
20/11/2012 06:04

kwa mara ya kwanza naweza kusema Tanzania imeamka, kwa matangazo bora na yenye kusisimua kama haya lazima tutatokomeza umasikini, ujinga na maradhi. Mungu awatangulie na kuwazidishia busara wale wote waliohusika kwanamna yoyote ila katika ufanikishaji wa matangazo haya.

Reply
ASM
20/11/2012 15:44

SIJUI NI NANI ANAWAFADHILI NATUMAINI ANAWAWEZESHA NA ANA LENGO LAKE ILA KAMA ANGEKUWA ANAWAJALI WATANZANIA VIZURI HUO UFADHILI ANGEGAWA HILO KUNDI LA VIJANA MAKUNDI MAWILI KUNDI MOJA LITUMWE CHINA NA LA PILI CUBA WAKAWAWAHOJI VIJANA WA NCHI HIZO WAMEWEZAJE KUPAMBANA NA UTANDAWAZI,UTANDAZUZU NA UTANDAWIZI MBONA KWAO HAWALII AJIRA,MBONA HAWALII NJAA ,MBONA WAO HAWALII MIKOPO YA ELIMU NA MAMBO MENGI WANGEWEZA HATIMAYE KUONDOA UMATI WA VIJANA MIJINI KWA JINA LA WAPIGA DEBE WAKAJITAFUTIE AJIRA ZENYE TIJA VINGINEVYO KAMPENI HIZO BADO NI UTANDAWAZI UNAENDELEA KUZAA UTANDAZUZU ILI UTANDAWIZI USISITISHWE SINA UHAKIKA IWAPO NIMEELEWEKA KUWA HUU BADO NI UBEBERU NA UKOLONIMAMBOLEO

Reply
K.L
22/11/2012 01:22

siyo ubeberu ila inajionesha wazi kuwa wewe ni mtu wa kupinga tu mambo na upo NEGATIVE na kwa hali kama yako inakuwa vigumu kwa taifa letu kuendelea mbele maana hata kama watu wanajaribu kufanya mambo mazuri kama matangazo haya, wewe utaona ni upuuzi na unaleta mfano wa Cuba!!!!!!

Reply
ASM
22/11/2012 08:56

NINA UGOMVI NA VIJANA WANAOISHI WALE BADALA YA KULA ILI WAISHI BILA JASHO HUNA HAKI YA KULA BILA WAJIBU HAKUNA HAKI KUPIGA DEBE SIO AJIRA POPOTE DUNIANI ILA UTANDAWAZI KABLA YA KUINGIA HATUA YA UTANDAWIZI UNAPITIA HATUA YA UTANDAZUZU SIKUSHANGAI NDIO RASILIMALIWATU TULIYONAYO TANZANIA

Alex
21/11/2012 04:06

Excellent!

Reply

Your comment will be posted after it is approved.


Leave a Reply