Letter from Barack Obama, U.S.A President : The beginning of the END of Operation Iraqi Freedom 01/09/2010
Friend -- Tonight marks the end of the American combat mission in Iraq. As a candidate for this office, I pledged to end this war responsibly. And, as President, that is what I am doing. Since I became Commander-in-Chief, we've brought home nearly 100,000 U.S. troops. We've closed or turned over to Iraq hundreds of our bases. As Operation Iraqi Freedom ends, our commitment to a sovereign, stable, and self-reliant Iraq continues. Under Operation New Dawn, a transitional force of U.S. troops will remain to advise and assist Iraqi forces, protect our civilians on the ground, and pursue targeted counterterrorism efforts. By the end of next year, consistent with our agreement with the Iraqi government, these men and women, too, will come home. Ending this war is not only in Iraq's interest -- it is in our own. Our nation has paid a huge price to put Iraq's future in the hands of its people. We have sent our men and women in uniform to make enormous sacrifices. We have spent vast resources abroad in the face of several years of recession at home. We have met our responsibility through the courage and resolve of our women and men in uniform. In seven years, they confronted a mission as challenging and as complex as any our military has ever been asked to face. Nearly 1.5 million Americans put their lives on the line. Many returned for multiple tours of duty, far from their loved ones who bore a heroic burden of their own. And most painfully, more than 4,400 Americans have given their lives, fighting for people they never knew, for values that have defined our people for more than two centuries. What their country asked of them was not small. And what they sacrificed was not easy. For that, each and every American owes them our heartfelt thanks. Our promise to them -- to each woman or man who has donned our colors -- is that our country will serve them as faithfully as they have served us. We have already made the largest increase in funding for veterans in decades. So long as I am President, I will do whatever it takes to fulfill that sacred trust. Tonight, we mark a milestone in our nation's history. Even at a time of great uncertainty for so many Americans, this day and our brave troops remind us that our future is in our own hands and that our best days lie ahead. Thank you, President Barack Obama SISIEMU Trans, oyaaa, unakwenda? 01/09/2010
Serikali ya Afrika Kusini imeongeza ahadi ya kiwango cha mshahara kwa zaidi ya milioni kwa wafanyakazi wa umma waliogoma. Rais Jacob Zuma alitoa wito wa kuanza upya mazungumzo baada ya mgomo huo wa wiki mbili kusababisha shule na hospitali nyingi kusimamisha shughuli zake. Baada ya kuwa na mjadala mzito usiku kucha, wawakilishi wa serikali wameongeza malipo hayo kwa asilimia 7.5. Vyama vya wafanyakazi vimekuwa vikitaka ongezeko la asilimia 8.6 na wanatarajiwa kupiga kura siku ya Jumanne usiku kuamua wakubali ongezeko hilo au la. Zwelenzima Vavi, katibu mkuu wa shirikisho kuu la vyama vya wafanyakazi, Cosatu, aliiambia BBC kuwa walipambana vilivyo katika mazungumzo hayo ili kuishinikiza serikali iongeze mshahara kwa asilimia nane. Alisema ni uamuzi wa wanachama iwapo watakubaliana na ongezeko hilo. "Jana usiku tulipambana vilivyo na mpaka kufika asubuhi haikuwezekana.. Nahisi itabidi mgomo kama huu wa takriban wiki moja au mbili ufanyike ndio Serikali itakubali matakwa yao." "Swali ambalo wanachama wetu wanatakiwa kujibu kwa sasa ni: je ni muhimu-ukizingatia masuala yote hayo- au ni hatua ya ushindi katika kipindi tulichofikia sasa?" Mgomo huu umeathiri zaidi mahospitali, ambapo wauguzi wa kijeshi na watu waliojitolea wakiendelea kuwahudumia wagonjwa. Takriban wafanyakazi wa umma milioni moja waligoma. Raisi Zuma amekuwa akikosolewa na wafanyakazi waliogoma kuwa alikuwa katika ziara ya kibiashara huko China, il hali wauguzi, walimu na wafanyakazi wengine wa umma apo mitaani wakitaka ongezeko la mishahara. Ilimbidi Raisi Zuma arejeshe mahusiano mazuri na vyama hivyo, ambavyo ni ngao muhimu, kabla ya kuwepo mkutano wa sera wa chama tawala, the African National Congress, katika kipindi cha wiki tatu. credit: BBC Swahili Najiuliza... ...ikiwa somo limeeleweka kwa Wafanyakazi wa Umma wa Tanzania na kwa Wananchi wasio Wafanyakazi wa umma lakini wanaotumia huduma za umma.. Raisi Mstaafu wa Tanzania awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa amezitaka nchi za Afrika kutoyumbishwa na propaganda za mataifa ya Magharibi kwamba wimbi la Wachina kuwekeza Afrika linaweza kuwafanya Waafrika kupoteza ardhi yao. Badala yake amezitaka nchi za Afrika kuweka mfumo mzuri wa majadiliano na Wachina, ili kushirikiana nao katika matumizi ya ardhi kwa lengo la kuzalisha kwa wingi na kukuza uchumi. ![]() Rais Mstaafu wa Tanzania Benjamin William Mkapa (kushoto) akimsikiliza Katibu Mtendaji wa African Forum Dk. John Tesha mara baada ya kumaliza mkutano wa Maraisi wastaafu na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam jana uliokuwa unaelezea mikakati ya maboresho ya ardhi barani Afrika. (photo: Mroki Mroki) “Msije mkababaishwa kwamba wawekezaji Wachina wana lengo la kuwanyonya na kuwanyang’anya ardhi Waafrika. Kinachotakiwa ni mpango mzuri wa kujadiliana nao na kuweka mfumo mzuri kwa manufaa ya kiuchumi,” alisema Mkapa baada ya marais wastaafu wa nchi za Afrika kumaliza mkutano wao Jijini Dar es Salaam jana. Mkapa alikuwa akijibu moja ya maswali yaliyoulizwa na waandishi wa habari kuhusu propaganda zinazoenezwa na mataifa ya Magharibi ya kuzihadharisha nchi za Afrika kuwa Wachina wanaweza wakawanyonya na hata kuchukua ardhi yao. "Jambo la muhimu nchi za Afrika zinapaswa kuchunguza na kujua ni mwekezaji gani ambaye ana uwezo wa kuleta mapinduzi ya kiuchumi haraka na kuwaletea wananchi maendeleo, na siyo kuangalia ni nani watashirikiana naye" alisema Mkapa. Akielezea mambo waliojadiliana kwenye mkutano huo, Rais Mstaafu wa Mauritus, Karl Offmann alisema suala la ardhi barani Afrika wameliona ni jambo nyeti ambalo linayumbishwa na misimamo mbalimbali ya kisiasa. Offmann alisema hawawezi kusema kwamba suala la ardhi Afrika halijatumika vizuri katika kuwaletea maendeleo Waafrika ila wana wasiwasi kasi ya ongezeko la watu, inaweza kuleta matatizo zaidi katika miaka ijayo. “Tunaposema idadi ya watu Afrika ni kubwa tunalinganisha na mabara mengine. Afrika imeonyesha kasi ya ongezeko la watu. Kwa mazingira hayo ni wazi matatizo yanaongezeka. Hali hiyo inaashiria kwamba sasa ni wakati wa kutatua matatizo yanayotokana na suala la umiliki wa ardhi,” alisema Offmann. Offmann alisema tatizo kubwa kwa nchi za Afrika ni kuweka usimamizi mzuri wa ardhi ni mawasiliano duni kama vile barabara na reli, hivyo masuala hayo, yanayopaswa kuwekewa kipaumbele. credit habari: Mwananchi ![]() Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Amani Abeid Karume (kulia) akishiriki kuimba wimbo wa taifa wa Tanzania wakati wa ufunguzi wa mkutano wa siku tatu wa Kikanda wa Kimataifa wa kukabiliana na ugaidi na uhalifu wa kimataifa leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Jaji Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Augustino Ramadhani. Mkutano huo unaendelea katika Hotel ya Golden Tulip na unahudhuriwa na Majaji kutoka ndani na nje ya Tanzania. Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustino Ramadhani amewaonya wanasiasa wanaozungumzia kesi mbalimbali zilizopo mahakamani, katika majukwaa ya siasa kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria za nchi. Jaji Ramadhani alitoa onyo juu ya kauli hizo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufunguliwa kwa semina ya siku tatu ya majaji wa mahakama za nchi 12 za Afrika. “Kesi zote zilizopo mahakamani hazitakiwi kuzungumziwa nje ya mahakama, mimi mwenyewe wakati kesi ya mgombea binafsi ilipokuwa mahakamani nilikuwa sitaki kuizungumzia nje ya mahakama,” alisema Jaji Ramadhani. Kuhusu hatua watakazochukuliwa watu wanaozungumzia kesi zinazoendelea mahamani, jaji Augustino alisema hawawezi kutoka mahakamani na kwenda kuwashika watu na kuwafungulia kesi bali mtu anatakiwa kupeleka malalamiko juu ya vitendo hivyo ndipo watakapoyafanyia kazi. Habari kamili ya semina ya siku tatu ya majaji wa mahakama wa nchi 12 za Afrika, isome katika Mwananchi Mgombea mwenza wa Profesa Ibrahim Lipumba anayewania nafasi ya urais kupitia CUF, Haji Juma Duni ameponda utaratibu unaotumiwa na CHADEMA pamoja na CCM ambavyo vinawasafirisha wagombea wao wa nafasi ya urais kwenda kuomba kura kwa wananchi kwa kutumia usafiri wa Helikopta. Aliviponda hivyo wakati wa mkutano wa Chama hicho wa uzinduzi rasmi kampeni za ubunge na udiwani mkoani Kagera ulifanyika kwenye viwanja vya uhuru vilivyoko ndani ya Manispaa ya Bukoba. Akiwa ameongozana na mbunge wa viti maalumu wa chama hichu mkoani Kagera, Savelina Mwijage na wagombea wa nafasi mbalimbali za ubunge na udiwani akiwemo mwanasiasa machachari Feliciani, alisema mgombea anayeomba kura kwa wananchi kwa kupitia angani kamwe hawezi kuelewa matatizo na kero zinazowakabili wananchi walioko chini ya ardhi na namna ya kuzitatua. Duni alisema hatua ya vyama hivyo ya kuwapitisha wagombea wao angani badala ya kuwapitisha chini ya ardhi inadhihirisha wazi jinsi gani vyama hivyo wasivyowajali wananchi wanaowaomba kura za kuwapa ridhaa za kuwaingiza ikulu. Aliwaambia wananchi kwenye mkutano huo wa hadhara kuwa kamwe CUF haitatumia utaratibu wa kuomba kura kwa kutumia helikopta, ijapokuwa CUF inao uwezo wa kuomba kura kwa kutumia helikopta. Aliendelea kusema kuwa CUF itaendelea kufanya kampeni zake kwa kutumia magari kwa kuwa matumizi ya magari yanakiwezesha chama hicho kitambue kwa urahisi kero na matatizo yanayawakabili wananchi,” ndugu wananchi huwezi kupitia angani ukaelewa kero zinazowakumba wananchi” alisema Duni. “Ndugu wananchi unapofanya kampeni kwa kupitia ardhini unapata uzoefu mkubwa sana, unaelewa kwa urahisi kero za barabara, unaweza kuelewa barabara zisizopitika na zinazopitika, wanaofanya kampeni kwa kupitia angani taarifa za kero zinazowakabili wananchi wanazisoma kwenye vitabu baada ya kuletewa”alisema mgombea huyo. Duni aliwaomba wananchi wakipe chama hicho ridhaa ya kuingia ikulu ili kiweze kutekeleza ilani yake vizuri, alisema ilani ya chama hicho inaeleweka na inaonyesha mwelekeo mzuri wa kuinua hali duni ya maisha waliyonayo Watanzania. Aliwaonya wananchi mkoani Kagera kuwa makini katika kuvichagua vyama vya kuongoza nchi, aliwaambia wasichague vyama ambavyo ni mali ya watu binafsi na ambavyo vinahubiri masuala ya udini na ukabila, alisema vyama hivyo ni hatari kwa maendeleo kwa kuwa vikiingia Ikulu vinaweza kufilisi nchi. “Kuna baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa wanaofikiri vyama wanavyoviongoza ni mali yao, ukitaka kuelewa vyama hivyo angalia viongozi hao wanavyoteuana, ikitokea nafasi mtu wa kwanza kufikiriwa lazima mjomba kwanza au shangazi au ndugu yoyote wa karibu na viongozi na wengine wanafikiriwa baadae, ndugu zangu kuweni makini na vyama hivyo msichague wagombnea wao” alimaliza. credit: Audax Mutiganzi, Bukoba via Michuzi post Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, amewachambua makada wa CHADEMA mmoja baada ya mwingine akiwemo Marando na Shibuda kwa akusema tuhuma zilizotolewa na CHADEMA ni matusi yasiyovumilika. Alisema, makada wote walioitukana CCM katika mkutano huo wa CHADEMA wapo katika kundi la watu wenye uelewa mdogo (Simple Mind People). ![]() Yufus Makamba / Katibu Mkuu CCM Kundi hilo ni miongoni mwa makundi matatu ya watu wenye uelewa na hivyo Makamba ana maana kwamba, viongozi wa Chadema wana akili ndogo. Aidha CCM imeitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kutosubiri barua ya malalamiko wakati chama kinapokiuka mwongozo wa maadili kwa vyama vya siasa, ichukue hatua kukiwajibisha chama kinachokiuka makubaliano hayo. Makamba ambaye alikuwa akizungumza kwa ucheshi alisema amelazimika kulizungumza hilo kwa kuwa yeye binafsi hawezi kuvumilia kuona kiongozi wao akitukanwa. “Hata kama ingekuwa ni wewe, unaona baba au mama yako anatukanwa, ungevumilia? Hakuna anayeweza kufanya hivyo na kama yupo dunia itamshangaa, kuna uvumilivu wa kisiasa unaokulazimu uvumilie chama kinapoguswa lakini si huu,” alisema Makamba. Alitaja uvumilivu huo wa kisiasa kuwa ni kuvumilia pale chama pinzani kinapokukosoa katika masuala ya elimu, kilimo, huduma za jamii lakini si katika kejeli na matusi kwa kuwa yanakwenda kinyume na mwongozo wa maadili ya vyama vya siasa ambao kila chama kinapaswa kuufuata. Makamba akisoma baadhi ya makatazo ya mwongozo huo alisema chama chochote hakitakiwi kufanya fujo, vurugu, kutumia lugha ya matusi, kashfa, kejeli, udhalilishaji au vitisho katika kampeni na kuongeza kuwa kinyume cha makatazo hayo, ndicho walichokifanya makada hao. Akimchambua kada John Shibuda, alisema, “eti (Shibuda) anasema CCM ni kama tairi bovu, sasa tujiulize, hivi tairi bovu ni nani kati yetu na yeye, Maswa (Jimbo alilokuwa akiliongoza kwa tiketi ya CCM) waligundua hili mapema, wakambwaga katika kura za maoni. “Kwanza baada ya kuona maji marefu, alikacha kugombea urais na kumsifia Kikwete kuwa ana maadili, anafaa tena akachangia Sh 200,000, leo anasema CCM gari bovu, kaishiwa hoja,” alisema. Kuhusu Marando alisema, “anapaswa amshukuru Kikwete, ninajua wenye kesi ya EPA si wakosaji bado ni watuhumiwa mpaka mwisho wa kesi, lakini hivi serikali ikamate watu hata kama ni tuhuma na wewe unawatetea, unatetea mafisadi?” Katibu huyo wa CCM alihoji kwa kuwa Dk Willibrod Slaa alishindwa kiapo cha kanisani cha upadri, hawezi kutunza kiapo cha kuongoza nchi. Amesema, hajali hata yeye (Makamba) akiwekwa katika kundi la wenye akili ndogo baada ya waandishi kuhoji kwa nini naye anazungumzia majina ya watu. source: TBC Redio za Tanzania 01/09/2010
Cross posting this from Candy1World blog whom I fully agree with here, and share the lamentations. Nimeamua kuongea kuhusu hili baada ya kuangalia CNN MultiChoice African Journalist Awards. I t is absolutely amazing seeing people making great stories, going to the source of the story, getting the untold and etc. Also the person who took the overall award of this year 2010, Sam Rogers, she was getting the story about the albino killings in Tanzania though I didn't get a chance to see the documentaryOur neighbours Kenya did well in the awards ceremony; not only Kenya but also Mozambique, South Africa and all others. When I switch on the radio and "tune", about 95% of all stations just do music. News will be read for about 5 minutes and it is done. Music is not the problem, the problem is Tanzanian radio stations [are] not interested in things happening around the world. Kama mambo yenyewe ndio hivyo, awards zitakuja kweli huku? Au ndio awards za hukuhuku za kumwaga?... Au ndio wanaona hizi redio za nje, namaanisha BBC au Deutsche Welle or VOA, wakileta habari zao ndio inatosha? I am just asking... Ujenzi unaendelea.... 01/09/2010
Ni ujenzi wa mengi. Ujenzi wa Demokrasia. Ujenzi wa kuitambua haki ya mwananchi. Ujenzi wa kujitambua tulikotoka, tuliko na tunakotakiwa kwenda. Ujenzi wa kufahamu umuhimu wa kushiriki kampeni na kumchagua kiongozi akufaaye. ...na ujenzi wa Nyumba ilee, ambao kwa sera nzuri, mjenzi anaweza kupata vitendea kazi bila ya ukiritimba. Taifa la Tanzania bado lipo katika Ujenzi, naam, kila leo twahimizwa, 'kulijenga Taifa'. picha zaidi za ziara ya kampeni ya Zitto Kabwe katika kijiji hiki zinapatikana katika blogu yake (bofya hapa) |