JINA LA KITABU: MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA BARA: TULIKOTOKA, TULIPO NA TUNAKOKWENDA Yaliyomo Kutabaruku............................... 7 Salamu za Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania ...................... 9 Shukrani.................................. 11 Dibaji....................................... 15 Utangulizi................................. 17 Vifupisho................................. 23 Sehemu ya Kwanza TANZANIA TULIKOTOKA 1. UKOLONI TANZANIA BARA.... 27 2. HARAKATI ZA UKOMBOZI...... 39 3. UHURU................................... 47 4. MAISHA BAADA YA UHURU... 57 Sehemu ya Pili TANZANIA TULIPO 5. JUBILEI YA MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA BARA.............. 69 6. JUBILEI NI KUANGALIA TUNU ZETU KAMA WATANZANIA..... 78 7. JUBILEI NA CHANGAMOTO ZETU....................................... 86 Sehemu ya Tatu TANZANIA TUNAKOKWENDA 8. JUBILEI NI KUANZA UPYA....107 9. KANUNI YA TIBA MCHEPUO KWA MAENDELEO YA TAIFA LETU....................................... 133 TATHMINI NA MOTISHA........ 145 HITIMISHO............................. 159 REJEA..................................... 169 MUHTASARI: Ndugu Watanzania wenzangu, nimendika kitabu hiki kwa malengo matatu. Kwanza kitabu hiki kinalenga kupanua mawazo na mtazamo wetu Watanzania kuhusu dhana ya Jubilei ambayo sisi tunafanya kumbukumbu ya miaka 50 ya uhuru wetu yaani kujua kuwa nini tunatakiwa tufanye. Uelewa huu utakuwa wa msingi kwa kizazi kitakachofanya Jubilei ya miaka 75 au miaka 100 ijayo ya taifa letu. Tena, lengo la pili la kuandika kitabu hiki ni kutoa uelewa ambao utakuwa ni chagizo la mabadiliko, ukombozi na maendeleo kwa watu tulioamua kutafakari na kutenda kadiri ya ukweli kwa manufaa ya taifa letu katika kizazi hiki na kijacho wakati huu tunapofanya Jubilei ya miaka 50 ya uhuru wetu. Na zaidi, lengo langu la mwisho la kuandika kitabu hiki ni kuchukua wajibu kama Mtanzania wa kushirikisha mawazo yangu kwa Watanzania wenzangu ili kuyatafuta maendeleo ya kweli ya taifa letu na zaidi sana ni kutoa mchango wangu katika sherehe hizi za taifa letu. Sikupenda sherehe kubwa kama hii ipite kama meli isiyoacha nyayo baharini. Kitabu hiki kimegawanyika katika sehemu kuu tatu. Sehemu ya kwanza ni Tanzania - tulikotoka ambayo inaongelea masuala ya ukoloni, harakati za ukombozi, uhuru na maisha baada ya uhuru. Sehemu ya pili inaongelea Tanzania – tulipo inayozungumzia hali yetu leo kiuchumi, kisiasa na kijamii nikijadili changamoto zetu kama taifa na tunu zetu tulizonazo tangu uhuru mpaka sasa kama Watanzania na maana na umuhimu wa sherehe zetu za Jubilei ya miaka 50. Hatimaye, sehemu ya tatu, inazungumzia Tanzania – tunakokwenda (mwanzo mpya) ikijadili wapi tunakokwenda kama taifa yaani kuwa na mwanzo mpya na kuingalia kanuni ya tiba mchepuo kama nyenzo ya kutufikisha huko. Kama yule mshairi na mtunzi wa vitabu wa Uingereza Robert Louis Stevenson alivyopata kusema kwamba, “Usipime siku yako kwa yale uliyovuna bali pima kwa yale uliyopanda.” Malengo hayo ndiyo yamenifanya nipande mbegu ya kitabu hiki kwa kuitakia mema nchi yangu kwa miaka 50 mingine. Mwisho natabaruku kitabu hiki ni kwa heshima ya taifa langu Tanzania linalofanya Jubilei ya miaka 50 ya uhuru wake na kwa namna ya pekee Mama yangu mpendwa Christina Shija, baba yangu mpendwa marehemu Gabriel Kasembo, marehemu babu yangu Chifu Yohana Kilangabhana Kasembo, marehemu bibi yangu Agatha Mija Michael, Hayati Askofu Mkuu Anthony Mayala, Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Watanzania wote ninaochangia nao utaifa na nia njema ya kuitakia mema nchi yetu na zaidi wenye moyo wa dhati wa kujenga taifa la Tanzania lenye heshima, upendo, amani na maendeleo ya kweli na ya uhakika kwa kizazi hiki na kijacho! Nakutakieni usomaji mwema na mafanikio tele katika maadhimisho ya jubilei ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania huku tu tukifakari uwepo, maisha na mustakabali wa taifa letu ! KWA KUAGIZA NAKALA YA KITABU HIKI ADIMU NA ADHIMU KWA TAIFA LETU, WASILIANA NA: JOHN MTWALE KASEMBO P.O BOX 22, PERAMIHO. SIMU: 0755 417 074 / 0712 120 775 BARUA PEPE: jmkasembo02@yahoo.com MWANDISHI: JOHN MTWALE KASEMBO, ni mzaliwa wa Mkoa wa Mwanza. Alisoma shule ya msingi Shamaliwa na baadaye masomo ya Sekondari kwenye Seminari za Nyegezi - Mwanza na Maua - Moshi. Ni mwezeshaji na mtoa mada wa mambo ya uongozi, dini, vijana, falsafa, ujasiriamali na amali za maisha. Ni mhitimu wa masomo ya falsafa na dini katika Chuo cha Mtakatifu Augustino Peramiho ambacho ni Chuo Kishiriki cha Chuo Kikuu cha Urbana, Roma. Pia. yeye ni mtafiti wa maendeleo ya Tanzania. Sasa anaendelea na masomo ya Shahada ya Kwanza ya Teolojia katika Chuo hicho hicho. Kitabu hiki kimechapishwa na kampuni ya Kolbe printing press, Nairobi nchini Kenya. Add Comment Serikali ya Tanzania imeufahamisha umma kuwa aliyekuwa kiongozi wa Libya ambaye sasa ni marehemu Muammar Qaddafi, binafsi hakuwahi kuwekeza kibiashara nchini Tanzania. Akijibu swali la Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi, aliyetaka kujua Tanzania inanufaika vipi na uwekezaji wa kanali Muammar Gaddafi kibiashara, na kwa kuwa Tanzania haitambui serikali ya mpito ya Libya ni nani anayesimamia uwekezaji wa kibiashara wa marehemu kanali Muammar Gaddafi; Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Mary Nagu amesema kumbukumbu za kituo za uwekezaji zinaonyesha mradi mmoja tu ulioandikishwa kutoka nchini Libya na kampuni ya NORTH AFRICA INVESTMENT TRADING COMMPANY na si wa marehemu Qaddafi. Akasema kampuni hiyo imeandika andiko la kibiashara la kuwekeza jumla ya dola za kimarekani milioni 5.8 na kutengeneza nafasi za ajira 160 pale ilipoinunua hoteli ya Bahari Beach iliyopo jijini Dar es Salaam. source Majaribu vumilia, naona yashindikana, Hasira zinanijia, furaha yakosekana, Hebu sasa fikiria, hawa wana wa rabana, Serikali na waganga, wapi mnatupeleka? Waganga mwajitahidi, roho zetu kuziponya, Hata sikuu ya Iddi, waganga mwapatikana, Kumbe nanyi mna dhiki, mnashindia makana! (pumba za mahindi au mtama) Serikali na waganga, wapi mnatupeleka? Maisha haya magumu, nani asiyeyajua, Waganga mwawahukumu, vinono mnajilia, Wapeni hata chandimu, nadhani watachezea, (mpira wa makaratasi) Serikali na waganga, wapi mnatupeleka? Wadanganyika fukara, Temeke twategemea, Msifanye masihara, sisi tunaangamia, Amana zetu nyembamba, hazitoshi enda Indya, (mshiko) Serikali na waganga, wapi mnatupeleka? Waganga namalizia, kama kweli mna nia, Wekeni chini SILAHA, pasiwe wa kubakia, Gogoro mwalirefusha, kwa kuwa mnapingana, Serikali na waganga, wapi mnatupeleka? Haya kama hayafai, basi jaribuni hili, Wote rudini kazini, mpunguze makaburi, Mola wetu si bahiri, pepo mtaikabiri, Serikali na waganga, wapi mnatupeleka? NA MGHANI WENU MZEE MTWANGAMBATE Dkt. Mtwangambate G.C; (M.D.) Kwa nini unanichora? 04/02/2012
Sizitaki hizo! Kwanza ni mbichi! 04/02/2012
Umewahi kufikwa na siku ambayo tangu mawio hadi machweo ya jua hakuna jambo moja unalofanya linaloelekea kufanikiwa bali ni vigingi, kero, karaha na maumivu tu? Nguruwe huyu kwenye video amenikumbusha siku hizo! Rais hakika naona aibu 04/02/2012
Nimepokea utenzi ufuatao kwenye email, simfahamu mtunzi, ila shukrani zote zimfikie. Rais hakika naona aibu, Sijui wewe una sababu, Umerudi uwe karibu, Huku madakitari wagoma. Rais umefika jana tu, Leo kutwa na viatu, Fungua benki ya watu, Huku madakitari wagoma. Rais nami umenchosha, Watu pia umewachosha, Sio siri hii inajionesha, Huku madakitari wagoma. Rais basi nenda Amana, Muhimbili napo umeona, Wagonjwa kila kona, Huku madakitari wagoma. Rais Bungeni Dodoma, Wanakula wao nyama, Muhimbili kumesimama, Huku madakitari wagoma. Rais hili tia makini, Sio za huku mijini, Hospitali za kijijini, Huku madakitari wagoma. Rais leo madakitari, Kesho pengine askari, Walimu nao wasubiri, Huku madakitari wagoma. Rais kemea hata hili, Achana na EPA na dili, Hayo sie tutasubili, Huku madakitari wagoma. Rais huko muhimbili, Wakudanganya ni shwali, Hakuna hata moja faili, Huku madakitari wagoma. Rais sema hata neno, Watanzania tuone upo, Kemea huyu we pepo, Huku madakitari wagoma. Naandika ushairi huu huku chozi linalengalenga, nilipita sehemu leo kuna mtu 1 alikuwa anaelezea ana mgonjwa Muhimbili mahututi anataabika toka mgomo uanza anakunywa pain killer. Rais amerudi ameishia enda kufungua FnB bank. Uwiiiii Mungu tusaidie sisi tusiojisaidia wenyewe pengine twaweza ona hata mwanga. Mungu ibariki Tanzania. Ndugu zangu, Mgomo wa madaktari wetu ni habari kubwa. Umeingia sasa kwenye wiki ya pili. Hata kama ungekuwa ni wa siku mbili, bado ungesababisha madhara makubwa kwa nchi. Kwamba sasa una zaidi ya siku kumi na nne ni balaa kubwa kwa nchi yetu. Tafsiri yangu; Uliopo ni mgogoro kati ya madaktari na Serikali. Na kwenye mgogoro kama huu, siku zote, wenye kuathirika zaidi ni wananchi walio wengi. Ni ukweli, kuwa karibu kila Mtanzania anayeamka asubuhi, ama ni mgonjwa au ana ndugu, jamaa au rafiki aliye mgonjwa. Hivyo basi, kuna mamilioni ya Watanzania wenye kutaabika kila siku na maradhi ya aina mbali mbali. Ni Watanzania wenye kutegemea sana huduma ya tiba inayotolewa na madaktari wetu. Na katika nchizetu hizi, daktari ni rafiki muhimu sana wa mwananchi. Ni jambo baya sana, pale Serikali inapoingia kwenye mgogoro na madaktari. Inapoingia kwenye mgogoro na marafiki wa wananchi. Hakuna mahali popote duniani wananchiwakatokea kuwachukia madaktari. Hivyo basi, ni balaa pia pale Serikali inaposhindwa kumaliza tofauti zake na madaktari wa wananchi kwa njia ya mazungumzo na hata kufikia hatua ya madaktari kugoma. Katika nchi zetu hizi, mganga wa tiba aliyesomeshwa kwa fedha za walipa kodi na kwa miaka mingi anahitajika sana. Mganga wa tiba msaidizi anahitajika sana. Na hata kama angelikuwapo Msaidizi wa Mganga Msaidizi wa tiba , naye angehitajika sana. Vivyo hivyo kwa wakunga wakuu na wasaidizi, wauguzi wakuu na wasaidizi wao. Wote hao anahitajika sana. Na katika nchi zetu hizi, Serikali hazipaswi kufikia hatua ya kuwatisha na hata kuwafukuza kazi madaktari. Hilo la mwisho lifanyike tu pale ambapo njia nyingine zote za kumaliza tofauti na kusuluhisha migogoro na madaktari zitakapokuwa zimeshindikana. Na kwanini ishindakane? Tufanye nini sasa? Taarifa kwamba Kamati ya kudumu ya Bunge inayohusika na masuala ya huduma za jamii imepanga kukutana na madaktari wetu ni hatua njema na ya busara. Maana, katika mgogoro huu taarifa zimekuwa zaidi za upande mmoja; upande wa Serikali. Ni wakati sasa pande zote mbili zikasikilizwa na Kamati hiyo ya Bunge. Ndio, ni wakati pia hata madaktari wetu wakapewa nafasi tuwasikie. Huu si wakati wa kufanya "propaganda" za kisiasa kwenye masuala ya afya za wananchi. Na hata pale Waziri wa Afya alipokaririwa jana Bungeni akitamka kuwa hali ya huduma za mahospitalini zimerejea katika hali yake ya kawaida ni mfano wa ’ Propaganda’ za kisiasa ambazo Watanzania hatuzihitaji kwa sasa. Hivi ni hali gani hiyo iliyorejea kwenye kawaida yake kwenye hospitali zetu baada ya mgomo huu wa madaktari unaoendelea sasa? Kwamba askari wetu wa Jeshi la Wananchi wamelazimika kwenda kutibu wagonjwa Muhimbili hiyo haiwezi kuwa ni ’ Hali ya kawaida’. Kwamba madaktari wameripoti lakini hawaonekani mawodini hiyo haiwezi kuwa ’ hali ya kawaida’. Na kama ni kawaida, hivi ni nini tafsiri ya ’ kawaida’? Hapa kuna ukweli unaopaswa kusemwa, na si kitu kingine bali ni ukweli. Watanzania tunataka kujua; ni kwanini watendaji wa Wizara husika wameshindwa kulitatua suala la madaktari wetu na hata kutufikisha hapa tulipo? Yumkini, kulikuwa na hali ya kuyapuuzia madai ya madaktari katika hatua za awali. Yawezekana pia watendaji wa Wizara hawakuwa karibu na wawakilishi wa madaktari hao ili kutoa fursa ya kuongea na kutafuta ufumbuzi wa tatizo. Labda ndio maana tumefika mahali sasa mgogoro umekomaa na wahusika kuonyesha hali ya kutunishiana misuli. Kuna mahali kosa limefanyika. Ni wapi? Ndio hapa, kuwa hata kama Kamati ya Bunge itafaulu kusuluhisha mgogoro huu, bado Watanzania tutahitaji iundwe Tume huru itakayochunguza namna watendaji wa wizara husika walivyolishughulikia suala hili kwa upande wao. Tume hiyo itusaidie kuupata ukweli mzima ili kama taifa, tujifunze. Na wakati tume kama hiyo itakapokuwa ikifanya kazi yake, itakuwa ni busara, kwa watendaji wakuu wa wizara husika wajiweke pembeni kwa maana ya kujiuzulu ili kupisha uchunguzi huo. Kama Tume itabaini kuwa hakukuwa na mapungufu makubwa katika utendaji wao na hususan walivyolishughulikia suala hili la mgogoro na madaktari, basi, itajulikana hivyo, na wana nafasi ya kurudi tena kwenye nafasi za utendaji Serikalini. Inahusu umma kurudisha imani yake kwa Serikali yao. Ndio maana ya umuhimu wa wahusika kupisha pembeni kuruhusu uchunguzi ufanyike. Maana, haitakuwa busara kuliacha suala hili likapita kama yanavyopita mengine ilihali limegharimu maisha ya Watanzania. Na kubwa zaidi kwa sasa, ni kwa pande zote katika mgogoro huu kutambua; kuwa kwa sasa mvutano unaoendelea hautatoa mshindi, ni kwa vile, katika kilichotokea na kinachoendelea kufanyika sasa, sote, kama taifa, tumeshindwa. Huu ni wakati wa kutanguliza busara na hekima. Tufanye yote, lakini, njia mujarab ya kutanzua mgogoro huu uliopo sasa ni mazungumzo katika mazingira ya kuheshimiana, basi. Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika. Maggid Mjengwa, Dar es Salaam, Jumamosi, Februari 4, 2012 mjengwablog.com These are the type of facebook-ers. 04/02/2012
Moto umewaka ndani ya kikao cha wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambapo wawakilishi hao walifikia hatua ya kutoa maneno makali dhidi ya Mwenyekiti wa chama hicho Rais Jakaya Kikwete. Wabunge hao wamesema hawaridhishwi na mwenendo wa serikali ya Rais Kikwete kiasi cha kufikia hatua ya kutishia kupiga kura ya kutokuwa na imani naye. Wabunge hao pia walipendekeza Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Haji Mponda, Naibu Waziri Dk. Lucy Nkya na Katibu Mkuu wa wizara hiyo Blandina Nyoni watimuliwe kwa kusababisha mgomo wa madaktari uliochangia kuongezeka kwa vifo vya wagonjwa waliokosa huduma za kitabibu katika hospitali mbalimbali nchini. Wabunge hao waliichachamalia serikali katika kikao cha ndani cha wabunge wa CCM, kilichofanyika katika ukumbi wa Pius Msekwa mjini hapa, chini ya uenyekiti wa Waziri Mkuu Mizengo. Vyanzo vyetu vya habari kutoka ndani ya kikao hicho vilisema kuwa pamoja na mambo mengine, wabunge hao walionyeshwa kukerwa na mambo mawili makubwa yaliyofanywa na Rais Kikwete na kusababisha wabunge wake wa CCM waonekane wajinga mbele ya wenzao wa upinzani, hususan Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Kwa mujibu wa habari hizo, mambo hayo ni pamoja na suala la posho mpya za wabunge na jinsi Rais Kikwete alivyoamua kumgeuka Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Spika wa Bunge, Anna Makinda, juu ya suala la posho za wabunge. Jambo jingine lililosababisha wabunge hao kumchambua Rais Kikwete ni suala la mabadiliko ya sheria ya Katiba ambapo mapendekezo mengi yaliyopitishwa na wabunge wa CCM bungeni yameondolewa baada ya Rais Kikwete kukubali mapendekezo ya CHADEMA. Endelea kusoma habari hii kwenye gazeti la Tanzania Daima | Vitabu vya WatanzaniaBofya picha ya kitabu unachokitaka ili ujinunulie nakala
Yaliyomo/CategoriesAll Hifadhi/ArchivesFebruary 2012 |






RSS Feed