Imeripotiwa kuwa wamiliki na wafanyabiashara katika maeneo ya mikoa mbalimbali nchini leo wamegoma kufungua maduka yao wakipinga uamuzi wa TRA wa kutaka kila duka liwe na mashine za EFD. Maduka yaliyokutwa yamefungwa asubuhi ya leo ni katika mitaa yote ya Kariakoo, Msimbazi, Uhuru, Lumumba, Aggrey, Mchikichi, Narung’ombe, Tandamti, Congo. Hali kadhalika, hali kama hiyo imeripotiwa kuwepo pia kwenye maduka ya mitaa ya miji ya Songea na Musoma.