Timka na Boda Boda yaacha neema kwa Watanzania

Mshindi wa promosheni ya Timka na bodaboda Bw. Ramadhani Abdallah akipiga kiki pikipiki yake tayari kuondoka nayo mara baada ya kukabidhiwa na Meneja Uhusiano wa Nje Salum Mwalim(kulia) katika tukio lililofanyika Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Dar es Salaam, Februari 19, 2014 -- Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania imejumuika na washindi wake 48 wa iliyokuwa Promosheni ya Timka na Bodaboda iliyodumu kwa kipindi cha miezi mitatu (3) kutoka Oktoba mwaka jana hadi Januari mwaka huu huku ikijivunia kuboresha maisha ya mamia ya Watanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania, Salum Mwalim amesema ni furaha kwa sababu wametimiza azma ya kubadili maisha ya Watanzania.

“Lengo letu lilikuwa ni kuja na promosheni itakayokuwa na zawadi ambazo zitabadili maisha ya wateja wetu, kutengeneza fursa za ajira na kuwategenezea vipato vya kuboresha maisha.” Alisema na kuongezea “Leo tunafuraha kuona kuwa lengo letu limetimia.”

“Ni azma ya wakati wote ya Vodacom kubuni na hatimae kuja na mambo mapya sokoni yatakayoendela kututofautisha sisi na wengine tukiakisi mahitaji ya wateja wetu moja kwa moja pamoja na kutengeneza fursa za kuyabadili maisha yao.” Alisema Mwalim.

Aliongeza kuwa kupitia promosheni hii, Vodacom wanajivunia kutoa Bodaboda 430 ambazo wateja wamejishindia sehemu mbalimbali za Tanzania. Hii ina maana kwamba kampuni hiyo imefanikisha malengo matatu ambayo ni pamoja na :- Kuchangia kustawisha maisha ya washindi na ya familia zao kwa kuwapatia vyombo vya usafiri kwani umuhimu wa bodaboda katika sekta ya usafiri kwa sasa hapa nchini kamwe haiwezi kupuuzwa.

Mwalim alisema “tumengeneza ajira nyingi kutokana na ukweli kwamba bodaboda hizi zinatumiwa kwa shughuli na malengo ya kibiashara. Wateja wetu ama wamejiajiri au kuajiri vijana wa kuziendesha na kuzisimamia kibiashara. Hivyo basi kwa wastani tu sio chini ya ajira 300 ambazo tumezitengeneza sehemu mbalimbali ya nchi kupitia washindi wetu”.

“Mbali na hapo, Vodacom imechangia kuleta unafuu na urahisi wa usafiri na usafirishaji. Kama tunavyotambua, bodaboda kwa sasa zimekuwa na msaada mkubwa katika kutoa huduma ya usafiri hasa maeneo ya vijijini na yaliyo pembezoni na miji. Ni wazi kwamba sio tu zimeleta riziki majumbani bali hata kuokoa maisha ya watu ambao wanapatwa na dharura zinazohitaji kukimbizwa hospitalini.” Alisema Mwalim.

Alihitimisha kwa kusema kuwa “Rai yetu kwa washindi wote ni kutambua thamani ya kile tulichowapatia kwa kuhakikisha kwamba wanazitunza pikipiki hizi ili ziweze kuwasaidia kwa kipindi kirefu zaidi huku. Pia nawaomba mzingatie matumizi salama ya Bodaboda ikiwemo sheria za usalama barabarani kila siku.”


 Meneja uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim akiongea na washindi wa promosheni ya Timka na bodaboda iliyomalizka hivi karibuni wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika Makako Mkauu ya Vodacom eneo la Mlimani City jijini Dar es Salaam.Jumla ya washindi 48 walikabidhiwa bodaboda zao zikiwa tayari zimeshasajiliwa.  

Sehemu ya pikipiki zikiwa tayari kutolewa kwa washindi wa promosheni ya Vodacom ya Timka na bodaboda iliyomalizika hivi punde. Pikipiki hizo zilikabidhiwa kwa washindi katika hafla fupi iliyofanyika Makao Makuu ya Vodacom yaliyopo Mlimani City jijini Dar es Salaam

Sehemu ya pikipiki 48 zikiteremshwa kwenye viunga vya Makao Makuu ya Kampuni ya Vodacom tayari kwa ajili ya zoezi la kukabidhiwa kwa washindi wa iliyokuwa promosheni ya timka na bodaboda iliyomalizika hivi karibuni na kuhusisha wateja wa Vodacom

Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim (wa kwanza kulia) akifuatilia zoezi la kuhakiki taarifa za washindi wa bodaboda wa iliyokuwa promosheni ya timka na bodaboda iliyomalizika hivi karibuni. (Kutoka kushoto) ni Ofisa Uhakiki wa Viwango wa Vodacom Ombeni Urasa, Regan Rugangira (mshindi) na Ofisa Masoko wa Vodacom Prestin Lyatonga. Jumla ya washindi 48 walikabidhiwa bodaboda zao kwenye hafla fupi iliyofanyika Makao Makuu ya Vodacom, Mlimani City jijini Dar es Salaam

Mshindi wa promosheni ya Timka na bodaboda Bw. Japhet Shedrack akiondoa pikipiki yake mara baada ya kuhakikiwa na (Kutoka kushoto) Ofisa Uhakiki wa Viwango wa Vodacom Ombeni Urasa, Ofisa Masoko wa Vodacom Prestin Lyatonga, Salum Mwalim Meneja wa Uhusiano wa Nje. Jumla ya washindi 48 walikabidhiwa bodaboda zao kwenye hafla fupi iliyofanyika Makao Makuu ya Vodacom, Mlimani City jijini Dar es Salaam