MV. Kigamboni kupelekwa matengenezoni

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA UJENZI

WAKALA WA UFUNDI NA UMEME(TEMESA)



Telegrams TEMESA DSM                                                            S.L.P  70704
Simu: +255-22-2862796/97                                                           DAR ES SALAAM
Fax:   +255-22-2865835                                                                TANZANIA



TAARIFA KWA UMMA

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) anawatangazia wananchi wote kuwa kivuko cha MV. Kigamboni kinatarajiwa kwenda kwenye matengenezo makubwa wakati wowote kuanzia leo.

Hivyo huduma za uvushaji zitaendelea kwa kutumia vivuko vya MV. Magogoni pamoja na MV. Lami katika kipindi chote cha matengenezo husika.

Uongozi wa TEMESA unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Imetolewa na Ofisi ya Mtendaji Mkuu

TEMESA
23/7/2014