Amri 10 za soka enzi zetu za utoto

Watoto wakisakata kabumbu huko Malindi Kenya kama walivyonaswa na kamera mwaka 2010 (picha: dreamstime.com)

Pamoja na sheria 17 za soka za FIFA kuwepo, enzi za utoto kulikuweko na sheria za soka ambazo ndizo zilizokuwa zinatambuliwa:-
  1. Mwenye mpira ndiye anayeamua nani atacheza
  2. Mtoto bonge ndiye golikipa
  3. Wachezaji mahiri ndio wanaochaguliwa kwanza
  4. Kukiwa na penati ruksa kubadilisha kipa
  5. Ukipiga mpira kwa nguvu au kwa mandochi mwenye mpira ana ruhusa ya kukuonya au kukukataza usicheze
  6. Usipochagia hela ya kujaza upepo utapigwa marufuku kucheza
  7. Hakuna marefa wala malinzmeni, na mpira unachezwa mpaka kuzunguka goli
  8. Kumkaba mwenye mpira faulo
  9. Ukitoboa mpira unalipa
  10. Mwenye mpira akikasirika au akiumia au akiitwa na mama yake ndio mwisho wa mechi

Imetoka kwa uncle John Kitime. Mtembelee kwenye blogu yake kwa vichekesho zaidi chekanakitime.blogspot.com