Vyumba vya Shule ya Sekondari ya Kiislam ya Mivumoni (Mivumoni Islamic Seminary) iliyopo ndani ya Msikiti huo vimeungua.
Eneo hilo ambalo lilikuwa likitumika kama mabweni ya Wanafunzi wa Shule hiyo, maabara na Ofisi za
Walimu limeteketea kabisa, hakuna kilichookolewa.
Othman Michuzi aliyekwenda kwenye eneo hilo amesema chanzo cha moto huo inadaiwa ni hitilafu ya umeme iliyokuwepo kwenye bweni la Wasichana Wanafunzi wa Shule hiyo.
Hakuna mtu yeyote aliepoteza maisha wala kujeruhiwa katika tukio hilo.
Picha zifuatazo ni kutoka kwa Othman Michuzi na Francis Dande...
Moto ukiunguza jengo la Msikiti waMtambani
Wananchi wakichota maji katika harakati za kusaidia kuzima moto.
Askari wakiimarisha ulinzi.
Mfanyakazi wa kampuni ya Altimate akiongeza maji kwenye kwa kutumia ndoo baada ya gari lao kuishiwa maji.
Gari la zimamoto likiwa limezungukwa na vijana waliokuwa wakisaidia zoezi la kuzima moto katika msikiti wa Mtambani Kinondoni.
Baadhi ya vijana wakisaidiana na wafanyakazi wa Kikosi cha Zimamoto kutoka kampuni ya Altimate Security kuweka maji katika gari baada ya gari hilo kuishiwa maji.
Moto ukishika kasi.
Moto ukienea katika eneo la juu.