Awamu ya pili: Wanafunzi wa kujiunga Kidato cha Tano 2014

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA TANO 2014
AWAMU YA PILI


Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa imetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano 2014 awamu ya pili.

Wanafunzi 8,101 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha tano awamu ya pili 2014, kati ya hao 4,987 wamepangwa tahasusi za sayansi ya jamii na biashara na wanafunzi 3,114 wamepangwa
tahasusi za sayansi.

Wanafunzi hawa wanatakiwa kuripoti kwenye shule walizopangiwa kuanzia tarehe 01 Septemba, 2014 na mwisho wa kuripoti ni tarehe 15 Septemba, 2014.

Imetolewa na Katibu Mkuu
OFISI YA WAZIRI MKUU – TAMISEMI
29 AGOSTI, 2014