Ndesamburo ambaye amechaguliwa kwenye nafasi hiyo kwa mara ya nne mfululizo, aliyasema hayo juzi mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa viongozi wa ngazi ya Mkoa.
- Basil Lema alifanikiwa kutetea nafasi yake ya Ukatibu wa Mkoa aliyoishikilia kwa vipindi viwili.
- Grace Kiwelu amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa BAWACHA
- Helga Mchomvu amechaguliwa kuwa Katibu BAWACHA.
- Samwel Msuya alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wazee.
- Eliakimu Kimaro amechaguliwa kuwa Katibu wa Baraza la Wazee.
- John Minja alichaguliwa kuwa Mweka Hazina wa Baraza la Wazee.
- Wawakilishi Baraza la Wazee Taifa ni William Maro na Ester Masiramba.
“Ukiona kiongozi anajipeleka mbele kujichagua huyo si kiongozi, anatakiwa aombwe na wananchi wanaoona anafaa kuwaongoza, na ikiwa hivyo kunakuwa hakuna masuala ya rushwa… mimi nilikuwa Ulaya, nimerudi nimekuta fomu, niwashuruku sana wazee wangu kwa kuniamini…
“Mliochaguliwa niwaombe mkafanye kazi ipasavyo, kiongozi mzuri anatafutwa na utatafutwa kwa kazi unayoifanya itakapoonekana na wale unaowaongoza, sasa hivi huko nje CCM wanalia wamepata taarifa Ndesa Pesa (Ndesamburo) kaingia tena,” alisema Ndesamburo ambaye pia ni muasisi wa CHADEMA.
Uchaguzi huo ulisimamiwa na Mwenyekiti wa Kanda ya Kaskazini, Mchungaji Israel Natse na Katibu, Amani Golugwa.