Makonda na mkewe watoa sadaka ya shukurani

Maombi yalifanyika kwake na mke wake ili Mungu amtangulie katika utumishi wake serikalini

Akitimiza mwaka mmoja tangu ateuliwe kuwa Mkuu wa Walaya Kinondoni, asubuhi ya Jumapili ya jana, Paul Makonda katika Ibada Kanisani Living Water Center Ministry Kawe alipokelewa kiroho na kumshukuru Mungu kwa kutoa sadaka ya shukrani kwa hatua aliyofikia.

Katika Ibada hiyo Mhe. Makonda ambayo aliongozana na mkewe, alipopewa nafasi ya kuzungumza alisema haikuwa raisi kwake ila Mungu amemuwezesha na kuwatia moyo, "usishindwe kufanya mambo ya kimaendeleo kwa changamoto za kimazingira au chochote," akisema kama ambavyo imekuwa ikionekana kwake.

Mapema akimkaribisha kuzungumza, Kiongozi wa Kanisa hilo Apostle Onesmo Ndegi alikuwa anaelezea jinsi ambavyo amemlea kiroho Mhe. Makonda hata kabla ya kuingia kuwa mtumishi wa serikali, jinsi alivyokuwa mbunifu wa shughuli mbalimbali na hivyo kinachofanyika leo sio kipya kwake na Bwana akatenda zaidi kwa kumfanya kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.


Apostle Onesmo Ndegi,Mke wake Lilian Ndegi na Mch. Peace Matovu wakifanya maombi kwa Mh. Makonda .



Mh. Paul Makonda alipokuwa akizungumza .

Kiongozi wa Kanisa la Living Water Centre Kawe Apostle Onesmo Ndegi

Apostle Onesmo Ndegi Kiongozi wa Kanisa la Living Water Centre alipokuwa akiwaeleza waumini kuhusu Mh. Paul Makonda

Apostle Onesmo Ndegi Kiongozi wa Kanisa la Living Water Centre alipokuwa akiwaeleza waumini kuhusu Mh. Paul Makonda .

Mh. Paul Makonda akiwa na Mke wake akimshukuru Mungu

Mh. Paul Makonda akiwa akifafanua jambo .