Ufafanuzi wa mapato na matumizi ya serikali Machi 2016

Waziri wa Fedha na Mipango, Philip Mpango akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa Wwizara ya Fedha jijini Dar es Salaam leo

UFAFANUZI WA MAPATO NA MATUMIZI YA SERIKALI KWA MWEZI MACHI, 2016


A: MAPATO 

(i) Mapato ya kodi (TRA) shilingi 1,283,274,000,000.

(ii) Mapato yasiyo ya kodi shilingi 77,504,000,000.

(iii) Mapato yatokanayo na vyanzo vya Halmashauri shilingi 43,490,000,000.

Jumla shilingi 1,404,268,000,000.

(iv) Tunatarajia pia kupata mikopo na misaada ya mifuko ya Basket na miradi ya maendeleo kutoka kwa washirika wa maendeleo shilingi 71,200,000,000.

B: MATUMIZI

1. Mishahara

(a) Watumishi wa Serikali Kuu na Serikali za Mitaa shilingi 484,057,177,680 ikijumuisha malimbikizo ya shilingi 9,479,389,384 na hasa kwa walimu katika Halmashauri 154.

(b)Watumishi wa Taasisi na Wakala za Serikali shilingi 97,985,822,320 ikijumuisha malimbikizo ya shilingi 518,822,320 kwa Taasisi na Wakala 24 na hasa sehemu kubwa Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Jumla ya mishahara ni shilingi 582,043,000,000.

2. Posho ya chakula kwa ajili ya vyombo vya ulinzi na usalama shilingi 43,556,500,000.

3. Ruzuku ya Vyama vya Siasa shilingi 1,433,583,000.

4. Posho ya Madaktari wanafunzi 1608 shilingi 1,721,000,000.

5. Wizara ya Afya Ununuzi wa madawa na vifaa tiba shilingi 2,597,961,000.

6. Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa semista ya tatu shilingi 57,040,000,000.

7. Kutekeleza mpango wa Elimu bure shilingi 18,777,000,000.

8. Mapato ya ndani kwa Halmashauri kwa ajili ya miradi na uendeshaji wa ofisi shilingi 43,490,000,000.

9. Madeni ya watumishi wasio walimu katika Halmashauri shilingi 3,618,900,612.

10. Miradi ya umeme shilingi 73,252,000,000.
- Wakala wa Umeme Vijijini shilingi 24,020,000,000.
- Mradi wa Umeme Kinyerezi I shilingi 43,800,000,000.
- Mradi wa kufua umeme makambako – Songea shilingi 5,482,000,000

11. Malimbikizo ya madeni ya Makandarasi wa barabara shilingi 166,905,919,730.

12. Miradi ya Maji shilingi 10,951,000,000.

13. Mfuko wa Reli shilingi 2,651,000,000.

14. Fidia kwa wananchi kupisha mradi wa Kurasini Trade and Logistic Hub shilingi 3,048,904,930.

15. Mradi wa Ununuzi wa dawa na vifaa Tiba (ORIO) shilingi 2,106,657,644.

16. Mfuko wa kuchochea maendeleo ya jimbo shilingi 5,124,997,500.