WM Majaliwa azindua duka la MSD wilayani Chato

Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu (kushoto), akitoa maelezo kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kabla ya kuzinduliwa duka la MSD

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amefungua dula la Bohari ya Dawa (MSD), la Wilayani Chato duka litakalotoa huduma kwa wananchi wa wilaya hiyo.

Akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa duka hilo Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu alisema duka hilo ni mfano kwa Wilaya nyingine na mikoa,ambapo tayari Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa (TAMISEMI mikoa na Wilaya kuanzisha maduka hayo, na kisha MSD itatoa ushauri wa kitaalam.

Bwanakunu alisema kwa kuanza,duka la dawa la Halmashauri ya Chato linaendeshwa na MSD, lakini baada ya muda watalikabidhi kwa Halmashauri ya Chato.


Waziri Mkuu Mhe.Kassim M. Majaliwa (wa tatu kushoto), akizungumza wakati akifungua dula la Bohari ya Dawa (MSD), Wilayani Chato.
  • Imeandaliwa na mtandao wa www.habarizajamii.com - simu namba 0712-727062)