Taarifa kutoka ndani ya Sahara Media Group Ltd, wamiliki wa StarTv, zimesema msimamo huo ulichuliwa na kiongozi wao mkuu Anthony Diallo jana na taarifa hizo zimethibitishwa leo kwa njia ya simu na Dk. Mwakyembe.
"Ni kweli nimeongea na Diallo, nimeelewa changamoto za kuongoza watu wengi na nimepokea apology yao, jambo ambalo ni uungwana.Wakati huohuo, Waziri huyo mwandamizi katika Serikali ya Awamu ya Tano amesema maandalizi ya kufungua kesi ya kashifa dhidi ya mmiliki, mhariri, mchapishaji na wasambazaji wa taarifa za uongo za gazeti hilo yanaendelea vizuri.
"Nimefarijika kuwa nao wametambua kuwa gazeti hilo halina viwango, hivyo hawatalisoma tena asubuhi", alisema Dk. Mwakyembe.