Lissu anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mnamo June 28, 2016 kwa kumuita ‘Mkuu wa Nchi ni dikteta uchwara’.
Baada ya kusomewa shtaka hilo Lissu amekana shtaka na kuachiwa huru kwa dhamana na hatotakiwa kusafiri nje ya nchi bila kibali cha mahakama.
Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa tena Agosti 02, 2016.