Maalim ahudhuria futari iliyoandaliwa na Tanzania Muslim Community Marekani

Katibu Mkuu wa chama cha wananchi (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad amewashukuru na kuipongeza Tanzania Muslim Community kwa juhudi zake za kufutarisha kila wiki ifikapo mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Maalim alihudhuria iftar siku ya Jumamosi, Juni 11, 2016 jijini Washington DC wakati akiwa katika ziara yake ya siku 14 nchini Marekani na Canada.



Mwenyekiti wa jumuiya kiislam ya watanzania inayounganisha majimbo matatu washington DC, Maryland, naVirginia (DMV) Sheikh Ali Mohammed, akitoa neno kwa waumini waliohudhuria, mbele ya mgeni rasmi Maalim Seif Shariff Hamad

Shamis Abdulla Mattar mmoja wa viongozi wa jumuiya akielezea machache

Mh. Jussa Ismail mmoja wa ujumbe ulioambata na Maalim Seif Shariff Hamad akisalimia na kutoa shukran wa Wanajumuiya

Mh. Maalim Seif Shariff Hamad kwa hisia kali akiwapondeza na kuwashukuru wana jumuiya na kuwataka waendelee na umoja walionao na mshikamano kwani huo ndio utamaduni wetu na muongozo wa dini, pia aliwaeleza atakuta na Watanzania siku ya Jumamosi

Sheikh Ibrahim alieyongoza sala ya magharib mbele ya waumin waliodhuria katika futari ya pamoja































































Ujumbe uliofuatana na Mhe Maalim Seif Sharif Hamad wakisikiliza kwa makini mawili matatu lutoka kwa maaalim Seif.
  • Picha zote: Vijimambo blog