Rais Magufuli ameitaka BoT kujiimarisha katika kusimamia maduka ya kubadili fedha za kigeni ambayo baadhi yake husafirisha fedha nje ya nchi na kutakatisha fedha haramu zikiwemo zinazotokana na dawa za kulevya.
Ametaka makampuni yanayowekeza kwenye madini kuondoka ikiwa kila mwaka kwa miaka nenda rudi, yanadai kuwa yanapata hasara lakini bado wanaendelea kuwepo. Amezitaka BoT na Hazina kushughulikia hilo.











Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli katika picha ya pamoja na Magavana na Manaibu Magavana na menejimenti ya BOT kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya benki kuu ya Tanzania kwenye ukumbi wa BOT jijini Dar es salaam Juni 22, 2016
