Akihojiwa katika televisheni ya Clouds, Lukuvi alisema sehemu kubwa ya Tanzania haipo katika mipango hivyo wanachokwenda nacho sasa ni kuipanga, kuipima na kuirasimisha.
“Mwaka 2016, kila Mtanzania mwenye ardhi ahakikishe anatafuta mpimaji wa ardhi aipime ardhi yake ili awe na hati,“ alisema Lukuvi.