
Vijana wa Bukoba Mpya wampongeza Prof Anna Tibaijuka kwa ushindi wa Tuzo ya 'HRH Prince Khalifa Bin Salman Al Khalifa Award for Suitanable Development.' Sherehe za utoaji wa tuzo hizo umefanyika juzi katika viwanja vya makao makuu ya umoja wa mataifa New York Marekani, na kuudhuriwa na viongozi mbalimbali duniani wakiwemo mabalozi, mawaziri kutoka nchi mbali na viongozi waandamizi wa Umoja wa Mataifa.

