Juzi nilisoma ujumbe wa "Mdau" kwenye mjengwablog.com, nikaunakili na kuuituma kwenye kundi pepe ambalo lina wadau wakuu wa hospitali husika kwa minajili ya kupata majibu ya dukuduku lililoelezwa katika ujumbe huo.

Niliyapata maelezo na kuyatuma kwa Mjengwa, na hapa nayarejea kama msisitizo.

DUKUDUKU

Mwenyekiti,

Habari gani za wakati, poleni kwa majukumu mengi.

Kwanza napenda kuwapa pongezi kwa kazi kubwa mnazozifanya za kuunganisha umma, kutoa habari za matukio muhimu kuchangia, mawazo N.K.

Nimesikishwa na habari niliyoisoma saa hii kuhusu hospital ya Mwana Nyamala.. kwa kweli sidhani kama binadamu yoyote pale mwenye akili timamu ambaye anaweza kufanya unyama wa namna hii, ya kumpa mgonjwa majibu ambayo sio sahihi na kwa makusudi kwasababu wagonwa ni wengi,.

Huu ni uuwaji, wote tunajuwa kuwa Malaria ina uwa ni hatari na pesa nyingi zinatumika kuutokomeza ugonjwa huu Africa au kupata chanjo kwa watoto,,uchunguzi ufanywe na ikindulika kuna ukweli ndali yake, wachukuliwe hatua kali za kisheria..

Mimi ni mtanzania maskini, ambaye naishi nje lakini kila mwaka narudi nyumbani napenda kushare kile ninachokipata kwa nguvu zangu, na ninapo kuwa nyumbani lazima nifike  ktk ward ya wototo ya occen road.

Mwaka jana nilipokuwa huko nikambiwa ward ya watoto imehamia Muhimbili tarehe 24 Dec nikaenda Muhimbili na kilichonipeleka tarehe hiyo ni kupata list ya orodha ambayo mtu unaruhusiwa kuwapelea wajonjwa, ambayo ni kawaida cha kushangasha kiufupi tu nilizunguushwa muhimbili pale masaa matatu, inchange wa hiyo ward yuko kwenye simu anaongea mambo binafsi,kamaliza ananimbia nenda kwa fulani, kifupi ni kwamba nimepigwa dana dana hadi nikapelekwa ofisi ya Agness Mtawa, mi simjuwi hapo palikuwa na kija anaitwa Maxwell whatever nae akawa kwenye simu pia, alipomaliza nika mwambia tafadhali naomba kujuwa utaratibu ili niweze kuleta msaada katika ward ya cancer ya watoto, jibu alilonipa ni unatakiwa kuandika barua ya maombi, nikamuliza maombi ya nini ?

Akasema maombi ya kibali,, nikamwambia napenda kufanya hivyo kesho xmas day, saa hii nielekeze jinsi ya kuiandika maana nimeshakuwa hapa masaa mawili na nusu. akasema ngoja nimpigie bosi wangu, akapiga simu kuongea na bosi wake ambaye  ni Agnes Mtawa, bosi akasema mwanbie afuate utaratibu. maombi kwa mkurugenzi wa afya na akipata kibali ndio atoe huo msaada. nilichoka maana inatia kichefu chefu, kwanini wasiniambie dakika kumi za mwazo ?? kwanini wanitembeze masaa matatu,nenda pale nenda pale, kwa mwendo huu hatutafika popote, hela yangu nimeipata kwa kufanya kazi hadi sekunde ya mwisho, napenda kusaidia watoto hospital maana humjuwi katoka mkoa gani, wala ni dini gani,, kama Mungu amekufisha salama xmas na wengine wako hospital kwanini tunapotaka kuwafariji wenzentu bado mnatuwekea masharti magumu, na kama
mtu anataka pesa bora akuambie kuliko kukuzungusha,, anyway naomba uongozi wa Idara zinazohusika waangalie hilo.

Ahsante
Mdau  

MAELEZO

Dear all
Hamjambo?

Nadhani ninyi nyote mmeona malalamiko ya huyu ndugu yetu aliyetaka kuja kutoa zawadi ward za  watoto muhimbili na akazungushwa. Mimi ninayeandika  ni huyo Agnes Mtawa asiyemfahamu.

Ninapenda tu kutoa angalizo kwamba tusiwe watu wa kulaumu tuu hata kama hatukufuata utaratibu.Ninavyojua mimi kila taasis inautaratibu wake ambao unapaswa kufuatwa. No matter hata kama unataka kutoa msaada. Msaada bila utaratibu haukubaliki. Huwezi  kutoka tu huko kwa sababu unauwezo wa kutoa msaada basi ukaingia taasisi au sehemu yoyote ile bila kibali. Nafikiri , kama Inafanyika huko kwingine basi hapa Muhimbili hallikubaliki.

Tumepewa dhamana ya kutoa huduma kwa  binadamu na siyo wanyama, ambao chochote kunachopelekwa au kutolewa kwao ni lazima yule aliyepewa dhamana ajiridhishe kwamba hicho kitu ni genuine, hakina madhara ndipo aruhusu kukitoa kwa wagonjwa.

Kwa hiyo badala ya kulaumu  ni vema ungeuliza na kufuata  utaratibu unaotakiwa kama policy ya Hospitali iliyo.
 
Sijui huko unakofanya kazi wewe kama wao hawana utaratibu,kwamba mtu anapojisikia tu kwenda kufanya chochote kile basi anaruhusiwa.

Kwa hilo sikubaliani na wewe.na imekuwa tabia na hasa kwa wenzetu mliobahatika kupata exposure  kwamba unapokwenda mahali bila utaratibu,na ukaelezwa utaratibu basi unahusisha na pesa na kujenga image mbaya sana kwa wenzenu. Nafikiri siyo sahihi hata kidogo. Ili kuepukana na fikra hizo potofu basi fuata utaratibu wa kuomba kibali, tena siku za kazi ili kweze kufanyiwa kazi na mhusika halisi ili uendelee na utaratibu uliyojipangia.
 
Agnes Mtawa
Mkurugenzi Huduma za uuguzi
Hospitali ya Taifa Muhimbili
P.O BOX 65,000
Dar es salaam
Tanzania

Email:agnes.mtawa@mnh.or.tz

Mobile:+255754629558
 
 
Picture
Wafanyakazi wa Shirika la ukaguzi na usimamizi wa vyama vya ushirika nchini –COASCO limemtaka mkurugenzi mkuu Severini Mosha na mkurugenzi wa fedha wa shirika hilo Hakimu Nyange kujiuzulu nyadhifa zao ndani ya siku saba kwa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha na kugawana raslimali za shirika kinyume na taratibu.

Wafanyakazi hao wa COASCO wametoa tamko hilo wakati wa mkutano wa baraza la wafanyakazi wa shirika hilo unaofanyika mjini Dodoma.

Hoja ya kutaka viongozi hao wajiuzulu ilitolewa na mwakilishi wa Shirika hilo kutoka mkoani Mbeya Alinabnuswe Mwakapala na kuungwa mkono na wajumbe waliohudhuria mkutano wa baraza hilo kwa kutia saini.

Katika hatua ambayo haikutarajiwa na wajumbe wa mkutano huo mmoja wa wajumbe hao Jeremiah Mgetwa kutoka mkoani Shinyanga alikataa kuunga mkono azimio hilo na ikalazimu wajumbe hao kumtoa nje ya mkutano kwa madai kuwa si mwenzao na hapaswi kuendelea kushiriki mkutano huo.

Wafanyakazi hao wameeleza kuwa maazimio hayo watayawasilisha kwa waziri wa kilimo chakula na ushirika na kwa waziri mkuu ili kushinikiza viongozi hao kuondolewa madarakani ili shirika lao liweze kusonga mbele.

Aneth Andrew,  TBC Dodoma.

 
 
Picture
House Minority Leader pictured standing, far right, speaks while colleagues play solitaire (imackgroup.com)
Picture
kibonzo kutoka: malickys.blogspot.com
 
 
Stop feeling lonely and depressed.

You are a strong, capable human being.

Why would you let someone else's words put you down?

Why would you allow someone to own you?

Be thankful for who you are and what you have. Look around and see how many people wish they had an opportunity like the one you have. Look around and see how many people wish they were you.

Stop wasting your time wishing for things to be the way they were for you can't have a better past. 

Enjoy the present moment. Embrace the power of now. It is what you do now that will set pace for a better tomorrow and the future. Do not wait for what tomorrow brings, instead, start working for it today, and now. You have all that it takes, you just need to stop feeling sorry for yourself and others. 

Move on and be thankful.

Let the circumstances be the stepping stone, not stopping stone.

If it wasn't meant to be, it will never be, no matter how hard you wish and hope. If it is meant to be it will, and on time, not before, not after, you can't rush it.
 
 
Picha hizi ni kwa hisani ya blogu ya Bin Zubeiry, tembelea  bongostaz.blogspot.com kwa picha zaidi za tukio hili.
Picture
Askari wa Usalama Barabarani akiongoza msafara wakati mwili wa marehemu, Mafisango ulikiwasili katika viwanja vya TCC Club
Picture
Prof. Sarungi akimpoza Ismail Aden Rage
Picture
Kocha wa Simba, Milovan Cirkovick
Picture
Beki wa Simba, Juma Nyoso pamoja na John Boko wakiwa wamebeba jeneza
 
 
 
 
Hii ni sehemu ya tau kati ya mfululizo wa mahojiano ya Mubelwa Bandio  na Mhe. Zitto Kabwe.

Katika sehemu hii, Zitto anayazungumzia Mashirika ya umma nchini Tanzania. Je! Yapo kwa faida ya wananchi?
Kama Mwenyekiti wa Tume ya Mahesabu ya Mashirika ya Umma anazungumzia vipi tatizo la TANESCO?
Ni nini kilisababisha shirika la TANESCO kufikia lilipo? Vipi wanajizatiti kuondoa hasara iliyolikumba? Ni vipi wana-diaspora wanaweza kushiriki katika kufufua TANESCO?

Ni wapi pa kuwekeza nchini?

Ukuaji wa miji na suala la mipango miji.

Kufuta vyeo vya Wakuu wa Mikoa na Wilaya.

Kwa nini kilimo ndiyo uti wa mgono japo kinazalisha kwa asilimia ndogo zaidi nchini? 

Ni vipi Tanzania inaweza kuondoka katika umaskini kwa muda mfupi?

Elimu ya Tanzania, inakua ama inaporomoka? 

AUDIO/SAUTI


VIDEO/VIDIO

 
 
The number of people using food stumps in the USA has increased partly due to the economic troubles of the past few years.

The U.S. Department of Agriculture reports that an average of 44 million people were on food assistance last year (that's up from 17 million in 2000). What might be surprising, though, is one subgroup that's taken a particularly hard hit.

The number of people with graduate degrees — master's degrees and doctorates — who have had to apply for food stamps, unemployment or other assistance more than tripled between 2007 and 2010, according to a report in The Chronicle of Higher Education.

In 2010, the report says, 360,000 of the 22 million Americans with graduate degrees received some kind of public assistance.

Chronicle reporter Stacey Patton spoke with Tell Me More host Michel Martin about why so many highly educated Americans have to rely on this type of aid.

Read more/Listen: The NPR.org
 
 
A new study has found out that the U.S. government spending to fight HIV/AIDS in developing countries is also preventing death from other diseases.

Some experts worry the billions of dollars the United States spends to treat people with HIV in poor countries may crowd out prevention and treatment of other illnesses but the findings of a study just published in JAMA, the Journal of the American Medical Association, suggest the opposite. The analysis indicates the President's Emergency Plan for AIDS Relief, or PEPFAR, has had substantial spillover benefits.

You can find more about the published study via this link (click here)