wavuti
 
Mtoto wa umri wa miezi mitatu wa Bwana Kim Yoo-chul, 41, na mkewe Choi Mi-sun, 25, wa nchini Korea amefariki dunia baada ya wazazi wake hao kumwacha bila huduma yoyote kwa mwendo wa saa 12 mfululizo.
Picture
random photo from the internet, not related to this story
Polisi wamesema kuwa wazazi hao walikuwa wakilea mwanasesere waliyempa jina la Anima kwenye programu ya Prius inayoendeshwa na 'Second-Life' kupitia kwenye tarakilishi (computer) iliyounganishwa na intaneti katika mgahawa mmoja nchini humo. Mchezo huo humpa mtu ruhusa ya kuwa na ndoto za Ali Nacha kuhusu kazi aipendayo, marafiki anaowapendelea na hatimaye hupewa zawadi za watoto kwa kushinda hatua moja ya mchezo kuelekea nyingine.

Wazazi hao waliporejea nyumbani siku moja baada ya kushinda kwa saa 12 mfululizo wakicheza mchezo huo, walikuta mtoto wao wa kweli, ambaye hakuwa na jina, amekwisha fariki na ndipo walipowapigia simu polisi ili kutoa taarifa hiyo. Uchunguzi uliofanywa ulibaini kuwa mtoto huyo alifariki kwa utapiamlo baada ya kukosa chakula kwa muda mrefu.

Inasemekana kuwa wazazi hao walikata tamaa ya maisha kwa kuwa hawakuwa na kazi huku wakiwajaaliwa(?) kuwa na mtoto njiti (mtoto aliyezaliwa kabla ya miezi tisa - a premature baby). Hivyo ili kupambana na hali halisi ya maisha iliyokuwa ikiwakabili, ndipo walipoamua kuucheza mchezo huo wa kulea mwanasesere hali iliyochangia kumsahau mtoto wa kweli aliyekumbwa na mauti.

YATOKANAYO
Ulevi wa matumizi ya tarakilishi na simu zilizounganishwa na intaneti unazidi kukua na kuathiri watu wa rika zote, hasa hasa vijana na watu wa umri wa makamo. Nimewahi kusikia visa vya wazazi kusemana na kulumbana juu ya mmoja wao kutumia muda mwingi kwenye simu (Blackberry, iPhone nk) katika nyakati nyeti kama vile wakati wa kula chakula, ambapo mtu anashindwa kushiriki chakula cha pamoja ama akishiriki basi muda mwingi anautumia kwenye simu badala ya kuzungumza na walioko mezani, wengine wanatumia muda mwingi msalani (uani, chooni) si kwa kuwa wanakwenda haja kubwa bali kwa kuwa wapo 'bize' na simu.

Wapo watu waliosababisha au kupatwa na ajali kutokana na matumizi ya simu zenye intaneti. Wengi wao wanapenda kusoma matukio ya papo kwa papo kwenye mitandao jamii kama vile Facebook au Twitter.

Hii ni changamoto kwetu sote kuwa makini na muda tunaoutenga katika kutumia intaneti ikiwa ni pamoja na kuwa makini na tovuti ama michezo tunayoipendelea. Ni vyema yeyote anayejiona kuwa muda wake mwingi unamegwa na intaneti, basi ajitahidi kujiwekea ukomo na kutafuta kitu mbadala cha kufanya ili kuondoa utegemezi uliopindukia wa intaneti.

Nadhani punde tutaanza kuwapata wasomi na wataalamu spesheli katika nyanja za matumizi ya intaneti na namna ya kupambana na ulevi wa matumizi ya intaneti. Tukifikia hapo, hata mmiliki wa tovuti hii, Subi, anahitaji kwenda 'internet rehab' - si utani.

 
 
Balozi mdogo wa Japani nchini Tanzania ambaye pia ni mtaalamu wa maswala ya uchumi, Yoshiyasu Mizuno ametembelea mvumbuzi wa jenereta la kutumia hewa kufua umeme.

Katika picha zifuatazo, balozi huyo anaonekana akiwa na mvumbuzi mwenyewe pamoja na wataalamu wengine kutoka Tanzania Industrial Research Development (TIRDO) eneo la Msasani ambapo ndipo lilipo jenereta hilo.
Picha kwa hisani ya blogu ya John Bukuku ya Full Shangwe.
 
 
Picture
Wakazi watatu wa mkoaniTanga, wawili wa Dar Es Salaam na raia mmoja wa nchini Iran wamekamatwa na madawa ya kulevya waliyokuwa wakiyaingiza nchini.

Bofya hapa ili kutizama kipande hicho cha habari kadiri kilivyorekodiwa na kuwekwa mtandaoni na Kennedy Kimaro wa blogu ya kennedytz.blogspot.com.

Tunatumai kwamba zoezi la kupambana na uingizaji wa madawa ya kulevya nchini Tanzania litaendelea kupewa kipaumbele kwani matumizi ya dawa za kulevya yamechangia kwa kiwango kikubwa sana kupumbaza vijana ambao ni nguvu kazi ya Taifa na kusababisha utegemezi mkubwa, jambo linalochangia kukua kwa kiwango cha umasikini miongoni mwa wananchi.

 
 
Kuna hili tukio la ukwapuaji wa kutumia gari ambao umekuwa ukishamiri sana hapa jijini kwa sasa,hivyo naomba uweke hapo mtaani kwetu ili wadau waweze kuwa makini na tukio kama hili. Kuna tukio limetokea hapa Sinza maeneo ya Mapambano njia ya nyuma kama unaenda Mwenge kwenye miti mirefu bar moja inaitwa kwa jimmy .

Kuna vijana 2 walikuwa wanatembea njiani mmoja kabeba begi lake la vitabu ghafla gari ndogo ikampitia kwa pembeni mtu aliyekwepo ndani ya gari akakwapua begi la yule kijana ambapo kulikuwa na simu na karatasi zake .

Huyo kijana alipiga kelele kidogo nilikuwa mbele yao nikajua labda ni tatizo lengine kumbe wenyewe wameibiwa bei lao kwahiyo ile saloon car nyeupe ikakimbia moja kwa moja

Kijana aliyeibiwa anaitwa Erick Thomas Jongela simu yake anasema ilikuwa na line 2 moja ni 0715 241204 na 0756 816 770 hizi line zilikuwa kwenye simu hiyo iliyokwepo kwenye begi lililoibiwa

Mwenzake mwenye simu anaitwa Fadhili no yake ni 0713 76 59 05 Kwa mtindo huu jamani muwe makini mnavyotembea na mabegi yenu pamoja na mali zingine zisivutie sana wahalifu hawa .

Nimetoa kisa Hichi kama tukio la kweli lililomkuta mtu naamini tigo pamoja na voda kwa kushirikiana na vyombo vya dola vitaweza kufuatilia simu ya kijana huyo na kuweza kupata taarifa zingine zinazohusiana na simu hiyo toka ilipozimwa mara ya mwisho.

Habari kwa mujibu wa blogu ya Othman Michuzi
 
 
Picture
 
 
Yule jamaa aliyenenepesha nyeti zake hadi kufikia zaidi ya kg10, Gasper Honza tayari amenza kupatiwa matibabu Nchini India, blogu ya Sufianimafoto inaandika.

Jopo la madaktari wa hospitali hiyo (jina kapuni mwa Sufianimafoto) tayari wameanza kufanya uchunguzi wa awali kwa kuchukua kipande cha nyama (biopsy) kutoka kwenye nyeti zake ili kubaini kemikali zilizokuwamo kwenye dawa aliyotumia.

Akizungumza na Sufianimafoto kwa njia ya simu jana kuhusiana na matibabu hayo, Gasper alisema tayari jopo hilo limempa dawa ya kupaka aina ya Hip absorb kwa ajili ya kupunguza uvimbe alionao kabla ya kumfanyia upasuaji katika nyeti yake.
“Kwa kweli tangu nimeanza kutumia dawa hii ninaona uvimbe unapungua japo napata haja ndogo chafu pamoja na maumivu makali, sina wasiwasi kwasababu nataka kupona hata hivyo daktaria wangu ameniambia nitapoteza nguvu za kiume jambo ambalo naona ni kawaida maadamu niutue mzigo huu,” alisema.

Kwa mujibu wa Dk. Hich Yagien wa India, Honza atapoteza uwezo wa nguvu za kiume baada ya upasuaji huo kutokana na uvimbe huo mkubwa kukaa kwa muda mrefu.
“Honza alifanya tofauti sana kwani dawa aliyotumia kwani dawa hiyo ni kwa ajili ya kukuza makalio ambayo zaidi hutumiwa na baadhi ya wanawake ingawa wengine waliotumia wameathirika na saratani na baadhi wamepoteza maisha baada ya upasuaji kutokana na kutokwa na damu nyingi. alisema daktari huyo.

Dawa hiyo ina nguvu sana na kwa mujibu wa maelezo ya dawa yenyewe mtu anatakiwa atumie mara mbili kwa wiki, lakini mtu anapoitumia bila kufuata masharti matokeo yake ni kama hayo ya kuvimba nyeti ama makalio bila mpngilio. ” alisema Dk. Yagien.
Alisema Honza atafanyiwa upasuaji mara baada ya vipimo kukamilika mwishoni mwa wiki hii.

Aidha alisema kuwa Honza si mgonjwa wa kwanza kukutana naye kwani ameshakutana na wagonjwa wa aina hiyo wengi tu ambao ameshawatibia kwa kuwafanyika upasuaji huku wengine wakifikishwa hospitalini hapo wakiwa wameoza.

Honza ambaye ni Mkazi wa Mbezi Beach Dar es Salaam, anatarajia kufanyiwa upasuaji huo wiki ijayo baada ya kutumia dawa ya kukuza makalio aina hypson akiwa na nia ya kukuza Nyeti ili kuinusuru ndoa yake Septemba mwaka jana.
 
 
Picture
Pata burudani hiyo kwenye ukurasa wa Audio (bofya hapa).

Nyimbo hizo zilizopo kwenye kaseti ya 'UKUMBUSHO' utunzi wake hayati Hemedi Maneti akiwa na Vijana Jazz Band ni:

SIDE A
1. Jiko limenuna
2. Najilaumu
3. Nilitaka iwe siri

SIDE B
1. Unikubalie
2. Ndoa ni kuvumiliana
3. Madaraka kwenye bar

Shukrani ya nyimbo: John B. mwenye blogu ya Likembe.

 
 
NAKONDE border in Northern Province was yesterday temporarily closed following a riot by irate Tanzanian traders that left three vehicles damaged.

The riot started at about 10:30 hours and by 12:00 hours both the Zambian and Tanzanian customs gates remained closed. An eye witness at the border said the riot was started by Tanzanian nationals who sell various merchandise on top of the Tanzania Zambia Railways (TAZARA) tunnel on the Zambian side after police confiscated their goods.

Police had been trying to prevent people from trading on top of the tunnel. The irate traders started throwing stones and all sorts of missiles at the combined team of council and state police as workers at the clearing agencies near the area scampered for safety. Three new vehicles were damaged in the process before a reinforcement of police officers arrived on the scene. Heavily armed police officers have since been deployed to keep vigil at the scene.

Nakonde district commissioner Billy Silwimba said the closure of the border was temporary. Silwimba said normal business was expected to resume anytime soon and that the confusion had been addressed. Silwimba, who described the riotous behaviour of the Tanzanian nationals as unfortunate, said importers and the local people should not panic as the situation was now under control.

Source: www.postzambia.com
 
 
Picture
Some of you have been looking for ways to save email addresses and contacts of your Facebook friends, however, there is no official way from facebook management on how to do that, but you can do a work around if you have a Yahoo or YMail address.

Here is how you do it:
  1. Login to your yahoo address account http://address.yahoo.com/?_src=&VPC=tools_export
  2. Click on the Facebook icon.
  3. Sign in with your Facebook username and password.
  4. You will see a notification with progress bar indicating the contacts being downloaded.
  5. After all is done, you will have all of your friend's contact addresses added in you Yahoo! address book.
You can import them to your gmail or hotmail or any other email account via a CSV file,j ust got to http://address.yahoo.com, download the file; then login to your account you want to export the contacts to and follow the instructions on how to import addresses from a CSV file (very simple). Gmail users, click here.

 
 
Picture